• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Kinondoni Municipal Council
Kinondoni Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Wasifu wa Halmashauri
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Afya na Usafishaji
      • Mipangomiji na Maendeleo ya Makazi
      • Kilimo na Mifugo
      • Elimu Sekondari
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA
    • Kata
      • Bunju
      • Hananasif
      • Kawe
      • Kigogo
      • Kijitonyama
      • Kinondoni
      • Kunduchi
      • Mabwepande
      • Magomeni
      • Makongo
      • Makumbusho
      • Mbezi Juu
      • Mbweni
      • Mikocheni
      • Msasani
      • Mwananyamala
      • Mzimuni
      • Ndugumbi
      • Tandale
      • Wazo
    • Muundo wa utawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya utalii
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Matukio ya Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo cha mijini
  • Huduma zetu
    • Biashara
    • Huduma za Elimu
    • Maji na Usafishaji
    • Ujasiriamali na utoaji wa mikopo
    • Ushauri katika Kilimo
    • Elimu ya ufugaji, mifugo na uvuvi
    • Vituo vya Ukusanyaji Mapato
    • Vibali vya Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomiji na Mazingira
      • Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Baraza la Madiwani
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Makala
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Fomu za maombi
    • Vibali vya Ujenzi Vilivyotolewa
    • Nyaraka za Elimu
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

WAZEE WAISHIO KINONDONI WAFUATWE KWENYE KATA KUANDIKISHWA ILI WAPATIWE KADI ZA MSAMAHA WA MATIBABU

Tarehe iliyowekwa: October 6th, 2017

  Wazee waishio  Wilaya ya Kinondoni wametakiwa kufuatwa kwenye Kata, Mitaa na maeneo wanayoishi ili waweze kutambuliwa kwa lengo la  kupatiwa kadi za msamaha wa matibabu. 

 Agizo hilo limetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mh Ali Hapi alipozuru katika kata ya Wazo na kukutana na wananchi wa mtaa wa kilimahewa kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika viwanjani hapo. 

 Amesema lengo la ziara yake ni ya kiserikali na kikazi pia, yenye nia ya kukutana na wananchi wa eneo husika kwa lengo la kusikiliza kero na changamoto zinazowakabili  ili ziweze kupatiwa ufumbuzi wa kudumu. 

 "Nimepewa kazi na Mh Rais, kwa hiyo nafanya kazi, hivyo niko hapa kama mtumishi wenu, ninyi ndio mabosi, Watendaji wanapaswa kujua kwamba ninyi wananchi ndio mmewaajiri na wanapaswa kutatua matatizo yenu, viongozi hatupaswi kuwa sehemu ya kutengeneza matatizo, viongozi tunapaswa kuwa sehemu ya suluhu ya matatizo,huo ndio uongozi bora ,na nilishasema tokeni ofisini, Mtendaji wa Kata, maafisa ugani wa kata watendaji wa Mitaa, tokeni ofisini nendeni kwa wananchi makasikilize shida zao ili muweze kuwapa maelezo na mipango ya Serikali kuhusiana na maeneo yao"amesisitiza Hapi 

 Amefafanua kuwa yapo mambo mengi ambayo Serikali imeyatilia mkazo hasa swala la matibabu ya bure kwa wazee na utekelezaji wake unaendelea vizuri. 

 "Nimewaagiza watendaji wangu, wafuateni wazee kwenye Kata na Mitaa yao, ili muweze kuwatambua, na kuwapatia kadi za msamaha wa matibabu, Serikali yetu imekwishasema wazee pamoja na watoto chini ya umri wa miaka mitano matibabu kwao ni bure, na hilo sina wasiwasi nalo kwa kuwa najua linatekelezeka "amesema Hapi 

 Amefafanua kuwa wazee ni hazina pekee tuliyonayo na hasa ikizingatiwa wameitumikia nchi yetu kwa kipindi chote hicho, hivyo yawapasa kutibiwa bure na hata wakati mwingine wasipange foleni. 

 Katika hatua nyingine amewataka wanachi kushirikisha Serikali pale inapotokea kuwepo na michango isiyoeleweka, isiyofuata utaratibu, wala kanuni za fedha ili matapeli hawa waweze kukomeshwa. 

 "Kuchangia maendeleo ni jambo zuri sana, na sisi tunahamasisha wananchi kuchangia maendeleo, lakini michango inautaratibu wake, nawaomba Sana pale mnapotaka kuchangia Jambo lenye nia ya maendeleo, washirikisheni viongozi wenu wa Serikali ili tujue na turizike, na wakati mwingine tujiridhishe kwamba lile mnalotaka kulichangia haliko kwenye mpango wa Serikali wa karibuni katika kulitekeleza "Amebainisha Hapi 

 Imetolewa na
 Kitengo cha Uhusiano
 Manispaa ya Kinondoni

Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI KWA VITENDO (PRACTICAL) June 30, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA VITENDO KWA NAFASI YA DEREVA DARAJA II June 29, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO ULIOFANYIKA TAREHE 28 JUNI, 2022 June 28, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 20, 2022
  • Tazama zote

Habari mpya

  • UHUSIANO WA DSM NA HAMBURG WAFANIKISHA UZINDUZI KIWANDA CHA MBOJI

    June 30, 2022
  • VIKUNDI 286 VYA WANUFAIKA WA MIKOPO YA ASILIMIA 10 VYAPATIWA MAFUNZO

    June 20, 2022
  • MAFUNZO KAZI YA MFUMO WA UTOAJI, USIMAMIZI WA MIKOPO YA ASILIMIA 10

    June 18, 2022
  • KINONDONI YAPONGEZWA KWA UJENZI WA KIWANJA CHA MICHEZO

    May 26, 2022
  • Tazama zote

Picha Jongefu

UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • TARATIBU ZA KUPATA KIBALI CHA UJENZI
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • UJASIRIAMALI NA UTOAJI MIKOPO
  • VITUO VYA KUKUSANYIA MAPATO
  • ORODHA YA WAHESHIMIWA MADIWANI
  • RATIBA YA MSTAHIKI MEYA
  • TAARIFA KWA UMMA
  • MIRADI ILIYOKAMILIKA

Viunganishi Linganifu

  • TOVUTI KUU YA IKULU
  • TOVUTI YA UTUMISHI
  • TOVUTI YA OR-TAMISEMI
  • TOVUTI YA OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • TOVUTI YA IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

Idadi ya Wasomaji

world map hits counter

Waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Morogoro, 14883 Dar es Salaam

    Anuani ya Posta: S.L.P 31902

    Simu ya mezani: +255 22 2170173

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: md@kinondonimc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni. Haki Zote Zimehifadhiwa.