• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Kinondoni Municipal Council
Kinondoni Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Wasifu wa Halmashauri
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Afya na Usafishaji
      • Mipangomiji na Maendeleo ya Makazi
      • Kilimo na Mifugo
      • Elimu Sekondari
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA
    • Kata
      • Bunju
      • Hananasif
      • Kawe
      • Kigogo
      • Kijitonyama
      • Kinondoni
      • Kunduchi
      • Mabwepande
      • Magomeni
      • Makongo
      • Makumbusho
      • Mbezi Juu
      • Mbweni
      • Mikocheni
      • Msasani
      • Mwananyamala
      • Mzimuni
      • Ndugumbi
      • Tandale
      • Wazo
    • Muundo wa utawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya utalii
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Matukio ya Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo cha mijini
  • Huduma zetu
    • Biashara
    • Huduma za Elimu
    • Maji na Usafishaji
    • Ujasiriamali na utoaji wa mikopo
    • Ushauri katika Kilimo
    • Elimu ya ufugaji, mifugo na uvuvi
    • Vituo vya Ukusanyaji Mapato
    • Vibali vya Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomiji na Mazingira
      • Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Baraza la Madiwani
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Makala
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Fomu za maombi
    • Vibali vya Ujenzi Vilivyotolewa
    • Nyaraka za Elimu
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Mifumo
    • NaPA
    • eMrejesho

KINONDONI YAPONGEZWA KUONGOZA MARA NNE MFULULIZO KIMKOA

Tarehe iliyowekwa: February 24th, 2020

NI KATIKA KUFANYA VIZURI KWENYE MATOKEO YA KIDATO CHA NNE CHA  PILI

 Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni ,imepongezwa kwa kufanya vizuri katika matokeo ya kidato Cha nne na cha pili kwa miaka minne mfululizo kwa mkoa wa Dar es Salaam.

Pongezi hizo zimetolewa na Afisa Elimu wa mkoa wa Dar es Salaam Bwana Hamis Lissu wakati wa hafla ya utoaji tuzo kwa walimu na shule zilizofanya vizuri kwa matokeo hayo kitaifa na kimkoa kwa mwaka 2019 ,2020.

Lissu amesema kuwa Halmashauri hiyo imekuwa ikifanya vizuri na kwa ufanisi mkubwa kwa kila eneo ikiwemo  Elimu, Afya na mazingira, Michezo na maeneo mengine na kusema kuwa mafanikio hayo yanatokana na kuwa na Mkurugenzi mwenye juhudi za kufanya kazi inayoendana na kasi ya Serikali ya awamu ya tano inayo ongozwa na Dk. John Pombe Magufuli.

Lissi amefafanua kuwa  Mkoa wa Dar es Salaam unajumla ya Halmashauri tano lakini Halmashauri ya Kinondoni inayo ongozwa na Mkurugenzi wake Aron Kagurumjuli imekuwa ikifanya vizuri katika sekta ya elimu ambapo imeongoza kuwa na matokeo mazuri kwa  miaka minne mfululizo katika mkoa huo.

" Kinondoni imekuwa ikifanya vizuri sana kwenye mambo mengi, binafsi mnanikosha na utendaji wenu uliotukuka ,niwasihi nguvu hii mliyokuwa nayo muendelee nayo ili kuendelea kuwa na rekodi nzuri kwa kuwa mfano bora kwa Halmashauri nyingine zilizopo katika mkoa wetu" amesema Bwana Lissu.

Lakini pongezi hizi pia zimuendee zaidi Mkurugenzi Kagurumjuli, Kinondoni mmepata Mkurugenzi bora, anafanya vizuri sana kwenye Halmashauri yake,na uchapakazi huu ndio anaoutaka Mhe. Rais wetu Dk. Magufuli, tukiwa na wachakazi kama hawa, hakika kwenye mkoa wetu tutakuwa na matokeo makubwa zaidi kwenye kila eneo” ameongeza Bwana Lissu.

Kwa upande wake Afisa Elimu Sekondari, wa Halmashauri hiyo, Bwana Leornad Msigwa  amesema katika matokeo ya kidato cha nne Kinondoni ilishika nafasi ya 39 kati ya Halmashauri 195 na hivyo kufanya kupanda nafasi tatu kitaifa ukilinganisha na mwaka 2018 ambapo ilishika nafasi ya 42 na kuendelea kuongoza kwa kishindo kwa miaka mine mfufulizo katika mkoa wa Dar es Salaam.


Msigwa ameongeza kuwa tathmini ya matokeo ya kidato cha nne  ya mwaka 2019 inaonyesha kuwa ufaulu umeongezeka kwa silimia 0.59 ukilinganisha na mwaka 2018 ambapo ufaulu umekuwa kwa asilimia 81.21 ambapo  mwaka 2019 ufaulu ulikuwa kwa asilimia 81.80.

 Kwa upande wa matokeo ya kidato cha pili , Msigwa ameeleza kuwa  tathmini ya upimaji wa matokeo ya kidato cha pili kwa mwaka 2019 , ufaulu ulikuwa kwa silimia 94.04 na hivyo kufanya Halmashauri ya Kinondoni kushika nafasi ya 24 kitaifa kati ya Halmashauri 184 na hivyo kupanda nafasi 10 kitaifa ukilinganisha na mwaka 2018.

Msigwa amefafanua kuwa, katika matokeo hayo  mwaka 2019 watahiniwa walikuwa 9,340 ambapo waliofaulu mtihani huo kati ya daraja 1-1V walikuwa 8,783 sawa na asilimia 94.04.

Amefafanua kuwa kati yao waliopata alama za ufaulu wa daraja la kwanza ni 1,682,  daraja la piIi ni  1,216, daraja la tatu 1,556, daraja la nne  4,329  huku jumla ya watahiniwa 557 walipata alama ya sifuri.

Katika hatua nyingine Msigwa amewaeleza walimu wa shule za Sekondari waliokuwa katika hafla hiyo kuendelea kujituma zaidi kwa kutumia mbinu mbalimbali za ufundishaji ili kuwezesha Halmashauri hiyo kuendelea kufanya vizuri zaidi kitaifa na kimkoa.

Imetolewa  na Kitengo cha Habari na Uhusiano

Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI May 24, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MWENYEKITI WA BODI YA AJIRA April 13, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA DEREVA DARAJA II September 21, 2021
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI (TAREHE 20 SEPTEMBA, 2021) September 21, 2021
  • Tazama zote

Habari mpya

  • KINONDONI YAPONGEZWA KWA UJENZI WA KIWANJA CHA MICHEZO

    May 26, 2022
  • BARAZA LA MADIWANI ROBO YA TATU KINONDONI LAFANYIKA LEO

    May 18, 2022
  • KINONDONI KUFIKIA WATOTO TAKRIBANI 156871 KAMPENI YA SIKU NNE CHANJO YA POLIO KITAIFA

    May 18, 2022
  • MWENGE WA UHURU KINONDONI 2022, WAPITIA MIRADI YENYE THAMANI YA SHILINGI TAKRIBANI BILIONI 3.9 FEDHA ZA KITANZANIA

    May 10, 2022
  • Tazama zote

Picha Jongefu

POSHO MADIWANI
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • TARATIBU ZA KUPATA KIBALI CHA UJENZI
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • UJASIRIAMALI NA UTOAJI MIKOPO
  • VITUO VYA KUKUSANYIA MAPATO
  • ORODHA YA WAHESHIMIWA MADIWANI
  • RATIBA YA MSTAHIKI MEYA
  • TAARIFA KWA UMMA
  • MIRADI ILIYOKAMILIKA

Viunganishi Linganifu

  • TOVUTI KUU YA IKULU
  • TOVUTI YA UTUMISHI
  • TOVUTI YA OR-TAMISEMI
  • TOVUTI YA OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • TOVUTI YA IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

Idadi ya Wasomaji

world map hits counter

Waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Morogoro, 14883 Dar es Salaam

    Anuani ya Posta: S.L.P 31902

    Simu ya mezani: +255 22 2170173

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: md@kinondonimc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni. Haki Zote Zimehifadhiwa.