• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Kinondoni Municipal Council
Kinondoni Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Wasifu wa Halmashauri
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Afya na Usafishaji
      • Mipangomiji na Maendeleo ya Makazi
      • Kilimo na Mifugo
      • Elimu Sekondari
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA
    • Kata
      • Bunju
      • Hananasif
      • Kawe
      • Kigogo
      • Kijitonyama
      • Kinondoni
      • Kunduchi
      • Mabwepande
      • Magomeni
      • Makongo
      • Makumbusho
      • Mbezi Juu
      • Mbweni
      • Mikocheni
      • Msasani
      • Mwananyamala
      • Mzimuni
      • Ndugumbi
      • Tandale
      • Wazo
    • Muundo wa utawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya utalii
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Matukio ya Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo cha mijini
  • Huduma zetu
    • Biashara
    • Huduma za Elimu
    • Maji na Usafishaji
    • Ujasiriamali na utoaji wa mikopo
    • Ushauri katika Kilimo
    • Elimu ya ufugaji, mifugo na uvuvi
    • Vituo vya Ukusanyaji Mapato
    • Vibali vya Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomiji na Mazingira
      • Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Baraza la Madiwani
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Makala
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Fomu za maombi
    • Vibali vya Ujenzi Vilivyotolewa
    • Nyaraka za Elimu
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

MAADHIMISHO YA WIKI YA UPANDAJI MITI YENYE KAULI MBIU ISEMAYO "TANZANIA YA KIJANI INAWEZEKANA, PANDA MITI KWA MAENDELEO YA VIWANDA " KIMKOA YAFANYIKA MANISPAA YA KINONDONI

Tarehe iliyowekwa: April 5th, 2018

 DC HAPI KWA NIABA YA MKUU WA MKOA WA DAR ES SALAAM AWA MGENI RASMI.-ASISITIZA UMUHIMU WA UPANDAJI NA UTUNZAJI WA MITI. 

 Maadhimisho ya wiki ya upandaji miti ngazi ya Mkoa, yameadhimishwa katika Manispaa ya Kinondoni kwa kupanda takriban miti 800 kwenye maeneo mbalimbali ya Mkoa huo ,kutoka katika vitalu vya wakala wa misitu (TFS) kwa kushirikiana na Halmashauri za Mkoa wa Dar es salaam.

 Akiongea katika maadhimisho hayo, yaliyofanyika katika Kata ya Kunduchi, Manispaa ya Kinondoni, Mkuu wa Wilaya hiyo, Mh. Alli Hapi kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam amesema siku hii ni muhimu Sana kwa wananchi kushiriki ili kwa pamoja tuweze kufikisha ujumbe mahususi kwa jamii kuhusiana na umuhimu wa upandaji miti, utunzaji na usimamizi wake. 

 "lengo ni kutumia siku hii maalum kufikisha ujumbe kwa jamii yetu, juu ya kuihamasisha Jamii katika swala zima la upandaji miti, utunzaji na usimamizi wake, na matumizi endelevu juu ya rasilimali zetu za misitu. "Amesema Hapi 

 Akifafanua kuhusiana na kauli mbiu ya mwaka huu isemayo "Tanzania ya Kijani inawezekana panda miti kwa Maendeleo ya viwanda" amesema ni muhimu Sana Tanzania yetu ya viwanda ikaendana na zoezi la upandaji miti kwani kwa kufanya hivyo itapunguza uharibifu wa tabaka la juu la anga(ozone) itokanayo na uzalishwaji wa hewa ya ukaa, ambapo uharibifu unapotokea husababisha miale ya moja kwa moja kushuka na kuumiza viumbe hai. 

 Ameongeza kuwa upandaji wa miti na utunzaji wa Mazingira ni ajira nzuri kwa vijana, kwani Mazingira yawapo mazuri na safi huwa vivutio kwa watu kupumnzika na kufanya shughuli zao .

 Aidha amezitaka Halmashauri zote za Mkoa wa Dar es salaam kuweka mifumo ya maji katika barabara zilizopandwa miti ili kuweza kurahisisha umwagiliaji. 

  Awali akitoa taarifa mbele ya Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, mwakilishi wa wakala wa huduma za  misitu nchini (TFS)  Bi Dyaga Follen Mkomwa, amesema siku hii ya upandaji miti kitaifa inatokana na waraka wa Serikali namba moja wa mwaka 2000 ,ambapo kila Wilaya nchini inatakiwa kupanda miche ya miti milioni moja na laki tano kila mwaka. 

 Ameongeza kuwa misitu iliyopo katika Mkoa wa Dar es salaam pamoja na upandaji huu wa miti ni jitihada za viongozi mbalimbali wa Serikali katika kusimamia utunzaji Mazingira, ambayo inasaidia kuboresha Mazingira na kufyonza hewa ukaa inayozalishwa viwandani kwa sasa, na pia kukabiliana na ongezeko kubwa la hewa ukaa itakayozalishwa kutokana na mkakati uliopo wa kuongeza viwanda katika Mkoa wa Dar es salaam. 

 Maadhimisho haya kimkoa yamehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa vyama na serikali kutoka katika Halmashauri zote za Mkoa wa Dar es salaam,  ambapo Kitaifa yanadhimishwa mkoani Shinyanga katika wilaya ya Kishapu.

 Imeandaliwa na
 Kitengo Cha habari na uhusiano
 Manispaa ya Kinondoni.

Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI KWA VITENDO (PRACTICAL) June 30, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA VITENDO KWA NAFASI YA DEREVA DARAJA II June 29, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO ULIOFANYIKA TAREHE 28 JUNI, 2022 June 28, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 20, 2022
  • Tazama zote

Habari mpya

  • UHUSIANO WA DSM NA HAMBURG WAFANIKISHA UZINDUZI KIWANDA CHA MBOJI

    June 30, 2022
  • VIKUNDI 286 VYA WANUFAIKA WA MIKOPO YA ASILIMIA 10 VYAPATIWA MAFUNZO

    June 20, 2022
  • MAFUNZO KAZI YA MFUMO WA UTOAJI, USIMAMIZI WA MIKOPO YA ASILIMIA 10

    June 18, 2022
  • KINONDONI YAPONGEZWA KWA UJENZI WA KIWANJA CHA MICHEZO

    May 26, 2022
  • Tazama zote

Picha Jongefu

UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • TARATIBU ZA KUPATA KIBALI CHA UJENZI
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • UJASIRIAMALI NA UTOAJI MIKOPO
  • VITUO VYA KUKUSANYIA MAPATO
  • ORODHA YA WAHESHIMIWA MADIWANI
  • RATIBA YA MSTAHIKI MEYA
  • TAARIFA KWA UMMA
  • MIRADI ILIYOKAMILIKA

Viunganishi Linganifu

  • TOVUTI KUU YA IKULU
  • TOVUTI YA UTUMISHI
  • TOVUTI YA OR-TAMISEMI
  • TOVUTI YA OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • TOVUTI YA IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

Idadi ya Wasomaji

world map hits counter

Waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Morogoro, 14883 Dar es Salaam

    Anuani ya Posta: S.L.P 31902

    Simu ya mezani: +255 22 2170173

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: md@kinondonimc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni. Haki Zote Zimehifadhiwa.