• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Kinondoni Municipal Council
Kinondoni Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Wasifu wa Halmashauri
  • Utawala
    • Divisheni
      • Miundombinu, Vijijini na Mijini
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Fedha na Mahesabu
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Manunuzi
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
    • Ofisi ya Mtendaji wa Kata
    • Ofisi ya Mtendaji wa Mtaa
    • Kata
      • Bunju
      • Hananasif
      • Kawe
      • Kigogo
      • Kijitonyama
      • Kinondoni
      • Kunduchi
      • Mabwepande
      • Magomeni
      • Makongo
      • Makumbusho
      • Mbezi Juu
      • Mbweni
      • Mikocheni
      • Msasani
      • Mwananyamala
      • Mzimuni
      • Ndugumbi
      • Tandale
      • Wazo
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fukwe na Visiwa
    • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
    • Matukio ya Utalii
  • Huduma zetu
    • Biashara
    • Huduma za Elimu
    • Ujasiriamali
    • Ushauri katika Kilimo
    • Vituo vya Ukusanyaji Mapato
    • Vibali vya Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomiji na Mazingira
      • Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba ya Meya
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Iliyopangwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Makala
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Mkataba wa huduma
    • Fomu za maombi
    • Vibali vya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Habari

MAADHIMISHO YA UKIMWI KIWILAYA YAFANYIKA KWA VITENDO KINONDONI

Tarehe iliyowekwa: December 1st, 2021

Akizingumza katika maadhimisho hayo yanayoenda kwa kauli mbiu ya Kitaifa isemayo "zingatia usawa, tokomeza UKIMWI,tokomeza magonjwa ya mlipuko" mgeni rasmi ambaye pia ni Naibu Meya wa Manispaa hiyo Mheshimiwa Kheri Misinga ameishukuru Serikali kwa kuweka hatua hii ya maadhimisho Kiwilaya kwani ni fursa pekee na ndio msingi imara wa kutathmini hali ilivyo sasa, tulikotoka na tunakokwenda hasa ikizingatiwa elimu katika suala hili la VVU na UKIMWI ni muhimu sana.

Amesema kuwa kufanyika maadhimisho haya pia ni kuimarika kwa demokrasia katika Halmashauri hali inayoleta ushirikiano katika kuhakikisha jamii inafikiwa kwa huduma zote muhimu ikiwemo elimu, afya na huduma za upimaji na chanjo.

Alipokuwa akitoa ufafanuzi wa hali ya upimaji na asilimia za maambukizi, Mganga Mkuu wa Manispaa hiyo Dkt. Samweli Laizer amesema hali imeendelea kuimarika na uelewa wa maambukizi ya VVU na UKIMWI kwa sasa ni mkubwa sana na kuwataka wananchi kutopuuza na kuhakikisha wanapima afya zao kabla ya kujihusisha na ngono zembe au kuingia katika mahusiano

Naye mratibu wa UKIMWI Manispaa ya Kinondoni Bi. Rhoby Gweso alipozungumza amesema lengo la kufanya maadhimisho eneo la Tandale uwanja wa sifa ni kufikisha elimu sahihi kwa wahusika na jamii kwa ujumla kuhusiana na madhara ya UKIMWI, ikiwa ni pamoja na kuwasisitiza umuhimu wa kutojihusisha na ngono zembe, pamoja na biashara ya kuuza miili yao.

Alipokuwa akisoma taarifa kwa niaba ya watu wanaoishi na virusi vya UKIMWI Kinondoni (WAVIU) ndugu Isakwisa Jeremiah amesema wanaishukuru Manispaa hiyo kwa kuwa mstari wa mbele kushirikiana nao hasa pale wanapohitaji msaada wa karibu ikiwa ni pamoja na kuiomba Serikali kuhakikisha  Afua za VVU na lishe zinaelekezwa kwa kundi maalumu la vijana kwani ndio walengwa wakubwa.

Maadhimisho hayo yaliyofanyikia katika Kata ya Tandale viwanja vya sifa yamehusisha wadau mbalimbali kama "Steps Tanzania", Care for AIDS, TAYOBECO, TAWIDO, YOP, PHSRF na MDH, ambapo shughuli mbalimbali zilifanyika ikiwemo kukabidhi misaada kwa WAVIU 52, upimaji wa VVU na chanjo ya UVIKO-19.

Kadhalika maadhimisho hayo pia yaliyohudhuriwa na wajumbe wa Kamati ya kudhibiti UKIMWI, Wakuu wa Idara na Vitengo pamoja na wadau wengine waliwasha mishumaa kama ishara ya kuwakumbuka wapendwa wao waliotangulia mbele za haki, lakini pia yalipambwa na burudani kutoka kwa msanii Salum Jabiri (Msaga Sumu), Bambo pamoja na Mtanga.

Imeandaliwa na

Kitengo cha Habari na Uhusiano.

Manispaa ya Kinondoni.

Matangazo

  • PONGEZI June 07, 2023
  • TANGAZO LA UUZAJI WA VIWANJA May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI-DEREVA DARAJA II April 24, 2023
  • MABADILIKO YA SIKU YA MAFUNZO YA WASIMAMIZI WA MAUDHUI, WASIMAMIZI WA TEHAMA NA MAKARANI WA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 July 28, 2022
  • Tazama zote

Habari mpya

  • AFISA ELIMU MSINGI KINONDONI APONGEZWA

    May 19, 2023
  • JAPAN YAIPATIA MSAADA MZIMUNI SEKONDARI

    March 15, 2023
  • VIKUNDI VYAASWA MATUMIZI SAHIHI YA MIKOPO

    February 18, 2023
  • "HAKUNA TIMU KUBWA ZAIDI YA KMC FC"

    February 18, 2023
  • Tazama zote

Picha Jongefu

VITUO VITANO VYA MSAADA WA MFUMO WA TAUSI, KITUO CHA MIITO YA SIMU KUBORESHA UKUSANYAJI WA MAPATO
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MWONGOZO WA NAMNA YA KUTUMIA MFUMO WA TAUSI
  • UJASIRIAMALI NA UTOAJI MIKOPO
  • TARATIBU ZA KUPATA KIBALI CHA UJENZI
  • TAARIFA KWA UMMA
  • RATIBA YA MSTAHIKI MEYA
  • ORODHA YA WAHESHIMIWA MADIWANI
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MIRADI ILIYOKAMILIKA

Viunganishi Linganifu

  • TOVUTI KUU YA IKULU
  • TOVUTI YA UTUMISHI
  • TOVUTI YA OR-TAMISEMI
  • TOVUTI YA OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • TOVUTI YA IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

Idadi ya Wasomaji

world map hits counter

Waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Morogoro, 14883 Dar es Salaam

    Anuani ya Posta: S.L.P 31902

    Simu ya mezani: +255 22 2170173

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: md@kinondonimc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni. Haki Zote Zimehifadhiwa.