• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Kinondoni Municipal Council
Kinondoni Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Wasifu wa Halmashauri
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Afya na Usafishaji
      • Mipangomiji na Maendeleo ya Makazi
      • Kilimo na Mifugo
      • Elimu Sekondari
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA
    • Kata
      • Bunju
      • Hananasif
      • Kawe
      • Kigogo
      • Kijitonyama
      • Kinondoni
      • Kunduchi
      • Mabwepande
      • Magomeni
      • Makongo
      • Makumbusho
      • Mbezi Juu
      • Mbweni
      • Mikocheni
      • Msasani
      • Mwananyamala
      • Mzimuni
      • Ndugumbi
      • Tandale
      • Wazo
    • Muundo wa utawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya utalii
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Matukio ya Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo cha mijini
  • Huduma zetu
    • Biashara
    • Huduma za Elimu
    • Maji na Usafishaji
    • Ujasiriamali na utoaji wa mikopo
    • Ushauri katika Kilimo
    • Elimu ya ufugaji, mifugo na uvuvi
    • Vituo vya Ukusanyaji Mapato
    • Vibali vya Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomiji na Mazingira
      • Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Baraza la Madiwani
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Makala
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Fomu za maombi
    • Vibali vya Ujenzi Vilivyotolewa
    • Nyaraka za Elimu
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

MAADHIMISHO YA UKIMWI KIWILAYA YAFANYIKA KWA VITENDO KINONDONI

Tarehe iliyowekwa: December 1st, 2021

Akizingumza katika maadhimisho hayo yanayoenda kwa kauli mbiu ya Kitaifa isemayo "zingatia usawa, tokomeza UKIMWI,tokomeza magonjwa ya mlipuko" mgeni rasmi ambaye pia ni Naibu Meya wa Manispaa hiyo Mheshimiwa Kheri Misinga ameishukuru Serikali kwa kuweka hatua hii ya maadhimisho Kiwilaya kwani ni fursa pekee na ndio msingi imara wa kutathmini hali ilivyo sasa, tulikotoka na tunakokwenda hasa ikizingatiwa elimu katika suala hili la VVU na UKIMWI ni muhimu sana.

Amesema kuwa kufanyika maadhimisho haya pia ni kuimarika kwa demokrasia katika Halmashauri hali inayoleta ushirikiano katika kuhakikisha jamii inafikiwa kwa huduma zote muhimu ikiwemo elimu, afya na huduma za upimaji na chanjo.

Alipokuwa akitoa ufafanuzi wa hali ya upimaji na asilimia za maambukizi, Mganga Mkuu wa Manispaa hiyo Dkt. Samweli Laizer amesema hali imeendelea kuimarika na uelewa wa maambukizi ya VVU na UKIMWI kwa sasa ni mkubwa sana na kuwataka wananchi kutopuuza na kuhakikisha wanapima afya zao kabla ya kujihusisha na ngono zembe au kuingia katika mahusiano

Naye mratibu wa UKIMWI Manispaa ya Kinondoni Bi. Rhoby Gweso alipozungumza amesema lengo la kufanya maadhimisho eneo la Tandale uwanja wa sifa ni kufikisha elimu sahihi kwa wahusika na jamii kwa ujumla kuhusiana na madhara ya UKIMWI, ikiwa ni pamoja na kuwasisitiza umuhimu wa kutojihusisha na ngono zembe, pamoja na biashara ya kuuza miili yao.

Alipokuwa akisoma taarifa kwa niaba ya watu wanaoishi na virusi vya UKIMWI Kinondoni (WAVIU) ndugu Isakwisa Jeremiah amesema wanaishukuru Manispaa hiyo kwa kuwa mstari wa mbele kushirikiana nao hasa pale wanapohitaji msaada wa karibu ikiwa ni pamoja na kuiomba Serikali kuhakikisha  Afua za VVU na lishe zinaelekezwa kwa kundi maalumu la vijana kwani ndio walengwa wakubwa.

Maadhimisho hayo yaliyofanyikia katika Kata ya Tandale viwanja vya sifa yamehusisha wadau mbalimbali kama "Steps Tanzania", Care for AIDS, TAYOBECO, TAWIDO, YOP, PHSRF na MDH, ambapo shughuli mbalimbali zilifanyika ikiwemo kukabidhi misaada kwa WAVIU 52, upimaji wa VVU na chanjo ya UVIKO-19.

Kadhalika maadhimisho hayo pia yaliyohudhuriwa na wajumbe wa Kamati ya kudhibiti UKIMWI, Wakuu wa Idara na Vitengo pamoja na wadau wengine waliwasha mishumaa kama ishara ya kuwakumbuka wapendwa wao waliotangulia mbele za haki, lakini pia yalipambwa na burudani kutoka kwa msanii Salum Jabiri (Msaga Sumu), Bambo pamoja na Mtanga.

Imeandaliwa na

Kitengo cha Habari na Uhusiano.

Manispaa ya Kinondoni.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI May 24, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA DEREVA DARAJA II September 21, 2021
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI (TAREHE 20 SEPTEMBA, 2021) September 21, 2021
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIKUNDI 286 VYA WANUFAIKA WA MIKOPO YA ASILIMIA 10 VYAPATIWA MAFUNZO

    June 20, 2022
  • MAFUNZO KAZI YA MFUMO WA UTOAJI, USIMAMIZI WA MIKOPO YA ASILIMIA 10

    June 18, 2022
  • KINONDONI YAPONGEZWA KWA UJENZI WA KIWANJA CHA MICHEZO

    May 26, 2022
  • BARAZA LA MADIWANI ROBO YA TATU KINONDONI LAFANYIKA LEO

    May 18, 2022
  • Tazama zote

Picha Jongefu

POSHO MADIWANI
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • TARATIBU ZA KUPATA KIBALI CHA UJENZI
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • UJASIRIAMALI NA UTOAJI MIKOPO
  • VITUO VYA KUKUSANYIA MAPATO
  • ORODHA YA WAHESHIMIWA MADIWANI
  • RATIBA YA MSTAHIKI MEYA
  • TAARIFA KWA UMMA
  • MIRADI ILIYOKAMILIKA

Viunganishi Linganifu

  • TOVUTI KUU YA IKULU
  • TOVUTI YA UTUMISHI
  • TOVUTI YA OR-TAMISEMI
  • TOVUTI YA OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • TOVUTI YA IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

Idadi ya Wasomaji

world map hits counter

Waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Morogoro, 14883 Dar es Salaam

    Anuani ya Posta: S.L.P 31902

    Simu ya mezani: +255 22 2170173

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: md@kinondonimc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni. Haki Zote Zimehifadhiwa.