• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Kinondoni Municipal Council
Kinondoni Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Wasifu wa Halmashauri
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Afya na Usafishaji
      • Mipangomiji na Maendeleo ya Makazi
      • Kilimo na Mifugo
      • Elimu Sekondari
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA
    • Kata
      • Bunju
      • Hananasif
      • Kawe
      • Kigogo
      • Kijitonyama
      • Kinondoni
      • Kunduchi
      • Mabwepande
      • Magomeni
      • Makongo
      • Makumbusho
      • Mbezi Juu
      • Mbweni
      • Mikocheni
      • Msasani
      • Mwananyamala
      • Mzimuni
      • Ndugumbi
      • Tandale
      • Wazo
    • Muundo wa utawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya utalii
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Matukio ya Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo cha mijini
  • Huduma zetu
    • Biashara
    • Huduma za Elimu
    • Maji na Usafishaji
    • Ujasiriamali na utoaji wa mikopo
    • Ushauri katika Kilimo
    • Elimu ya ufugaji, mifugo na uvuvi
    • Vituo vya Ukusanyaji Mapato
    • Vibali vya Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomiji na Mazingira
      • Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Baraza la Madiwani
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Makala
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Fomu za maombi
    • Vibali vya Ujenzi Vilivyotolewa
    • Nyaraka za Elimu
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

KINONDONI YAZINDUA KAMATI YA MAAFA YA WILAYA.

Tarehe iliyowekwa: November 22nd, 2018

Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mh Daniel Chongolo leo,  amezindua kamati ya maafa ya Wilaya yenye wajumbe 29 ambapo wajumbe 18 ni kutoka timu ya Manispaa na wajumbe  11 ni wadau kutoka nje ya Halmashauri, hafla iliyofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Manispaa.

 Akizindua kamati hiyo, Mkuu huyo wa Wilaya katika hotuba yake amesema,  maafa ni tukio kubwa linalotokea na kuathiri utaratibu wa maisha ya jamii na kusababisha madhara makubwa kwa watu, mali, uchumi na mazingira  ambapo huzidi uwezo wa jamii kukabiliana nalo.

 Ameongeza kuwa kwa Serikali kutambua uwepo wa maafa na majanga Nchini na umuhimu wa kukabiliana nayo,  imetunga sheria ya usimamizi wa maafa namba 7 ya mwaka 2015, inayotaka uundwaji wa kamati ufanyike, kwa lengo la kuchukua hatua za kujiepusha nayo na kukabiliana pindi yanapojitokeza.

 Amesema "Kamati ninayoizindua leo ni utekelezaji wa matakwa ya Sheria, hivyo hatupo hapa kwa bahati mbaya na kamati hii inatambulika kwa mujibu wa sheria tajwa, kifungu cha 15 na 16 hivyo nendeni mkafanye kazi" Amesisitiza Chongolo.


 Awali akisoma taarifa ya uundaji wa kamati ya usimamizi wa Maafa wa Wilaya kwa niaba ya Mkurugenzi wa Manispaa,  Mratibu wa Maafa wa Manispaa hiyo Bi.Pendo Fred amewataja wajumbe wanaounda kamati kuwa ni wakuu wa idara na vitengo 16 vya Manispaa, Jeshi la zimamoto na uokozi Mkoa wa Kinondoni, TARURA, TANESCO, DART,  DAWASCO na vyombo vya habari.

 Aidha ameainisha mipango na mikakati ya kamati kwa mwaka 2018/2019 kuwa ni kufanya mkutano na wadau, kutoa mafunzo kwa kamati za maafa ndani ya Mtaa na Kata, kuanzisha program ya kutoa mafunzo katika jamii na Halmashauri kutekeleza miradi ya DMDP kwa kujenga barabara zenye mifereji.

 Naye mratibu wa timu ya wataalam ya uokoaji ya Mkoa wa Dar es Salaam (DARMAERT),  Ndg Christopher Mzava, alipokuwa akitoa taarifa yake ameyaainisha majukumu ya kamati iliyozinduliwa kuwa ni kuhuisha masuala ya dharura na maafa katika mipango ya maendeleo, kufuatilia tishio la majanga na maafa na kufanya uchunguzi wa kutokea kwa maafa na uchoraji wa ramani.

 Nyingine ni kuainisha mahitaji ya mafunzo kwa umma na kutoa elimu, kutafuta rasilimali na kusimamia operesheni za maafa na kuunda timu ya ukabilianaji wa maafa na muundo wa kulinda jamii.

 Uzinduzi wa kamati hiyo pia umehudhuriwa na wawakilishi kutoka Bank ya Dunia, msalaba mwekundu, wawakilishi kutoka ofisi ya Mkuu wa mkoa na waheshimiwa madiwani.

 Imeandaliwa na
 Kitengo cha Habari na Uhusiano.
 Manispaa ya Kinondoni.

Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA VITENDO KWA NAFASI YA DEREVA DARAJA II June 29, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO ULIOFANYIKA TAREHE 28 JUNI, 2022 June 28, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MWENYEKITI WA BODI YA AJIRA April 13, 2022
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIKUNDI 286 VYA WANUFAIKA WA MIKOPO YA ASILIMIA 10 VYAPATIWA MAFUNZO

    June 20, 2022
  • MAFUNZO KAZI YA MFUMO WA UTOAJI, USIMAMIZI WA MIKOPO YA ASILIMIA 10

    June 18, 2022
  • KINONDONI YAPONGEZWA KWA UJENZI WA KIWANJA CHA MICHEZO

    May 26, 2022
  • BARAZA LA MADIWANI ROBO YA TATU KINONDONI LAFANYIKA LEO

    May 18, 2022
  • Tazama zote

Picha Jongefu

POSHO MADIWANI
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • TARATIBU ZA KUPATA KIBALI CHA UJENZI
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • UJASIRIAMALI NA UTOAJI MIKOPO
  • VITUO VYA KUKUSANYIA MAPATO
  • ORODHA YA WAHESHIMIWA MADIWANI
  • RATIBA YA MSTAHIKI MEYA
  • TAARIFA KWA UMMA
  • MIRADI ILIYOKAMILIKA

Viunganishi Linganifu

  • TOVUTI KUU YA IKULU
  • TOVUTI YA UTUMISHI
  • TOVUTI YA OR-TAMISEMI
  • TOVUTI YA OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • TOVUTI YA IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

Idadi ya Wasomaji

world map hits counter

Waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Morogoro, 14883 Dar es Salaam

    Anuani ya Posta: S.L.P 31902

    Simu ya mezani: +255 22 2170173

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: md@kinondonimc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni. Haki Zote Zimehifadhiwa.