• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Kinondoni Municipal Council
Kinondoni Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Wasifu wa Halmashauri
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Afya na Usafishaji
      • Mipangomiji na Maendeleo ya Makazi
      • Kilimo na Mifugo
      • Elimu Sekondari
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA
    • Kata
      • Bunju
      • Hananasif
      • Kawe
      • Kigogo
      • Kijitonyama
      • Kinondoni
      • Kunduchi
      • Mabwepande
      • Magomeni
      • Makongo
      • Makumbusho
      • Mbezi Juu
      • Mbweni
      • Mikocheni
      • Msasani
      • Mwananyamala
      • Mzimuni
      • Ndugumbi
      • Tandale
      • Wazo
    • Muundo wa utawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya utalii
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Matukio ya Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo cha mijini
  • Huduma zetu
    • Biashara
    • Huduma za Elimu
    • Maji na Usafishaji
    • Ujasiriamali na utoaji wa mikopo
    • Ushauri katika Kilimo
    • Elimu ya ufugaji, mifugo na uvuvi
    • Vituo vya Ukusanyaji Mapato
    • Vibali vya Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomiji na Mazingira
      • Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Baraza la Madiwani
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Makala
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Fomu za maombi
    • Vibali vya Ujenzi Vilivyotolewa
    • Nyaraka za Elimu
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Mifumo
    • NaPA
    • eMrejesho

KINONDONI YAUNGANA NA HALMASHAURI NYINGINE KOTE NCHINI KUADHIMISHA KILELE CHA WIKI YA MAZINGIRA CHENYE KAULI MBIU ISEMAYO "MKAA NI GHARAMA TUMIA NISHATI MMBADALA "

Tarehe iliyowekwa: June 5th, 2018

Manispaa ya Kinondoni leo wameungana na Halmashauri nyingine kote nchini , kusherehekea kilele cha maadhimisho ya wiki ya Mazingira chenye kauli mbiu isemayo "Mkaa ni gharama, tumia nishati mmbadala ", kwa kuonesha bidhaa zao kupitia wajasiriamali waliowezeshwa yakilenga kuinua uchumi wa viwanda.

Katika maadhimisho hayo yaliyofanyika Kitaifa katika viwanja vya mnazi mmoja, jijini Dar es Salaam, ambapo mgeni rasmi wake akiwa Makamu wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mh Samia Suluhu Hassan yalilenga kutoa elimu na uelewa juu ya utunzaji na Uthamini wa Mazingira, ambapo yalipambwa kwa burudani za kiasili pamoja na shughuli za ujasiriamali zilizokuwa zikioneshwa uwanjani hapo.

Katika hotuba yake Mama Samia suluhu amewataka watanzania kuelewa athari zitokanazo na ukataji wa miti kiholela na kuhakikisha wanakuwa walinzi wa kwanza wa Mazingira hayo.

Amezitaja athari hizo kuwa ni kukimbiza wanyama, kupoteza matunda ya asili, kuharibu makazi ya wadudu wenye kazi mbalimbali, kuharibu misitu inayotusaidia kunyonya joto au hewa ukaa na bahari kuingia eneo la makazi ya watu.

Naye Waziri wa Nchi ofisi ya Rais Mazingira Mh. Januari Makamba alipokuwa akimkaribisha Makamu wa Rais amesema siku hii ambayo huadhimishwa 05/06 kila mwaka ni siku ya kuhakikisha uelewa unakuwepo kwa watanzania ya kwamba maendeleo huenda sambasamba na utunzaji wa mazingira hivyo ni wajibu wa kila mwananchi kusimama kwenye nafasi yake kwa swala hilo.

Akitoa salamu za Mkoa wa Dar es salaam, Mkuu wa Mkoa huo Mh Paul Makonda amesema zipo changamoto zinazoukabili Mkoa wake, na kuzianisha kuwa ni swala la mafuriko, pamoja na uchafu uliokithiri na kutangaza tarehe 01/07/2018 kuwa siku maalumu ya operesheni ya usafi kwenye Mkoa wake.

Maadhimisho hayo yamehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa vyama na Serikali ,watumishi kutoka Halmashauri za Mkoa wa Dar es salaam pamoja na mikoa ya jirani, yaliyoenda sambamba uoneshaji wa bidhaa za wajasiriamali pamoja na utoaji wa tuzo za ushindi wa utunzaji wa Mazingira.


Imeandaliwa na

Kitengo cha Uhusiano Manispaa ya Kinondoni

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MWENYEKITI WA BODI YA AJIRA April 13, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA DEREVA DARAJA II September 21, 2021
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI (TAREHE 20 SEPTEMBA, 2021) September 21, 2021
  • TANGAZO LA KUWAPANGA WAFANYABISHARA KATIKA MAENEO RASMI September 28, 2021
  • Tazama zote

Habari mpya

  • BARAZA LA MADIWANI ROBO YA TATU KINONDONI LAFANYIKA LEO

    May 18, 2022
  • KINONDONI KUFIKIA WATOTO TAKRIBANI 156871 KAMPENI YA SIKU NNE CHANJO YA POLIO KITAIFA

    May 18, 2022
  • MWENGE WA UHURU KINONDONI 2022, WAPITIA MIRADI YENYE THAMANI YA SHILINGI TAKRIBANI BILIONI 3.9 FEDHA ZA KITANZANIA

    May 10, 2022
  • MEYA KINONDONI AFUTURISHA

    April 27, 2022
  • Tazama zote

Picha Jongefu

POSHO MADIWANI
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • TARATIBU ZA KUPATA KIBALI CHA UJENZI
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • UJASIRIAMALI NA UTOAJI MIKOPO
  • VITUO VYA KUKUSANYIA MAPATO
  • ORODHA YA WAHESHIMIWA MADIWANI
  • RATIBA YA MSTAHIKI MEYA
  • TAARIFA KWA UMMA
  • MIRADI ILIYOKAMILIKA

Viunganishi Linganifu

  • TOVUTI KUU YA IKULU
  • TOVUTI YA UTUMISHI
  • TOVUTI YA OR-TAMISEMI
  • TOVUTI YA OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • TOVUTI YA IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

Idadi ya Wasomaji

world map hits counter

Waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Morogoro, 14883 Dar es Salaam

    Anuani ya Posta: S.L.P 31902

    Simu ya mezani: +255 22 2170173

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: md@kinondonimc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni. Haki Zote Zimehifadhiwa.