• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Kinondoni Municipal Council
Kinondoni Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Wasifu wa Halmashauri
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Afya na Usafishaji
      • Mipangomiji na Maendeleo ya Makazi
      • Kilimo na Mifugo
      • Elimu Sekondari
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA
    • Kata
      • Bunju
      • Hananasif
      • Kawe
      • Kigogo
      • Kijitonyama
      • Kinondoni
      • Kunduchi
      • Mabwepande
      • Magomeni
      • Makongo
      • Makumbusho
      • Mbezi Juu
      • Mbweni
      • Mikocheni
      • Msasani
      • Mwananyamala
      • Mzimuni
      • Ndugumbi
      • Tandale
      • Wazo
    • Muundo wa utawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya utalii
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Matukio ya Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo cha mijini
  • Huduma zetu
    • Biashara
    • Huduma za Elimu
    • Maji na Usafishaji
    • Ujasiriamali na utoaji wa mikopo
    • Ushauri katika Kilimo
    • Elimu ya ufugaji, mifugo na uvuvi
    • Vituo vya Ukusanyaji Mapato
    • Vibali vya Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomiji na Mazingira
      • Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Baraza la Madiwani
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Makala
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Fomu za maombi
    • Vibali vya Ujenzi Vilivyotolewa
    • Nyaraka za Elimu
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Mifumo
    • NaPA
    • eMrejesho

KINONDONI YASAINI MKATABA WA LISHE, KWA LENGO LA KUTEKELEZA SERA YA LISHE KWA VITENDO

Tarehe iliyowekwa: November 9th, 2018

Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni, katika utekelezaji wa sera na maelekezo ya Wizara  ya Afya maendeleo ya Jamii Jinsia wazee na watoto na OR-TAMISEMI imesaini mkataba wa lishe utakaotumika kutekeleza mapango jumuishi wa lishe wa Kitaifa(NMNAP) wa mwaka 2016-2017/2021, kwa watoto wenye umri chini ya miaka mitano.

Akisaini mkataba huo kati yake na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mh.Daniel Chongolo,  Mkurugenzi wa Manispaa hiyo  Ndg Aron Kagurumjuli amesema Manispaa yake iko tayari na imejipanga vizuri kuanza ukurasa mpya wa utekelezaji wa afua za lishe kwa ufanisi na kwa vitendo,  na kwa kuzingatia mahitaji ya mkataba huo, kwani kwa kufanya hivyo itakua imeenda sambamba na uboreshaji wa afya ya mtoto mwenye umri chini ya miaka mitano,  kwa kumpatia lishe bora na yenye afya kwa mujibu wa  miongozo, sera, na kanuni katika kufikisha tija inayokusudiwa.

Akifafanua mahitaji yaliyoko katika sera hiyo ya lishe,  Mganga Mkuu wa Manispaa hiyo Dkt. Festo Dugange amesema Sera hiyo inasisitiza kila Halmashauri kutenga bajeti ya kiasi cha tsh 1000/=kwa kila mtoto wa umri chini ya miaka 5, kutoka mapato ya ndani, kwa lengo la kutekeleza shughuli za lishe kwenye maeneo ya kipaumbele.

Ameyataja maeneo hayo ya kipaumbele kuwa ni  watoto kupata vyakula vyenye virutubisho sahihi na kwa kiasi kinachostahili, kuhakikisha elimu ya lishe inatolewa kikamilifu kwa wajawazito na watoto wenye umri chini ya miaka mitano, kuhakikisha watoto wenye utapiamlo mkali wanapatiwa matibabu stahiki, na kufanya kaguzi za vyakula hasa chumvi zenye madini  joto.

Nyingine ni kuhakikisha wajawazito wanapatiwa madini chuma na vidonge vya Foliki Acid ili kuzuia upungufu wa damu na matatizo yanayosababishwa na ukosefu wa madini hayo kwa watoto, kutekeleza vikao vya Halmashauri vya kamati ya lishe kila robo kwa lengo la kufanya tathmini ya hali ya lishe na kuhakikisha wanashirikiana na wadau mbalimbali wa lishe walioko katika Halmashauri kwa lengo la kufanikisha.

Hafla hiyo ya kutiliana saini mkataba huo iliyofanyika katika ofisi ya Mkuu wa Wilaya,  imehudhuriwa pia na Katibu tawala wa Wilaya hiyo Bi. Stella Msofe, na Afisa lishe wa Manispaa hiyo Bi. Emiliana Sumaye

Imeandaliwa na

Kitengo cha Uhusiano na Habari.

Manispaa ya Kinondoni.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MWENYEKITI WA BODI YA AJIRA April 13, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA DEREVA DARAJA II September 21, 2021
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI (TAREHE 20 SEPTEMBA, 2021) September 21, 2021
  • TANGAZO LA KUWAPANGA WAFANYABISHARA KATIKA MAENEO RASMI September 28, 2021
  • Tazama zote

Habari mpya

  • BARAZA LA MADIWANI ROBO YA TATU KINONDONI LAFANYIKA LEO

    May 18, 2022
  • KINONDONI KUFIKIA WATOTO TAKRIBANI 156871 KAMPENI YA SIKU NNE CHANJO YA POLIO KITAIFA

    May 18, 2022
  • MWENGE WA UHURU KINONDONI 2022, WAPITIA MIRADI YENYE THAMANI YA SHILINGI TAKRIBANI BILIONI 3.9 FEDHA ZA KITANZANIA

    May 10, 2022
  • MEYA KINONDONI AFUTURISHA

    April 27, 2022
  • Tazama zote

Picha Jongefu

POSHO MADIWANI
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • TARATIBU ZA KUPATA KIBALI CHA UJENZI
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • UJASIRIAMALI NA UTOAJI MIKOPO
  • VITUO VYA KUKUSANYIA MAPATO
  • ORODHA YA WAHESHIMIWA MADIWANI
  • RATIBA YA MSTAHIKI MEYA
  • TAARIFA KWA UMMA
  • MIRADI ILIYOKAMILIKA

Viunganishi Linganifu

  • TOVUTI KUU YA IKULU
  • TOVUTI YA UTUMISHI
  • TOVUTI YA OR-TAMISEMI
  • TOVUTI YA OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • TOVUTI YA IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

Idadi ya Wasomaji

world map hits counter

Waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Morogoro, 14883 Dar es Salaam

    Anuani ya Posta: S.L.P 31902

    Simu ya mezani: +255 22 2170173

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: md@kinondonimc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni. Haki Zote Zimehifadhiwa.