• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Kinondoni Municipal Council
Kinondoni Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Wasifu wa Halmashauri
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Afya na Usafishaji
      • Mipangomiji na Maendeleo ya Makazi
      • Kilimo na Mifugo
      • Elimu Sekondari
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA
    • Kata
      • Bunju
      • Hananasif
      • Kawe
      • Kigogo
      • Kijitonyama
      • Kinondoni
      • Kunduchi
      • Mabwepande
      • Magomeni
      • Makongo
      • Makumbusho
      • Mbezi Juu
      • Mbweni
      • Mikocheni
      • Msasani
      • Mwananyamala
      • Mzimuni
      • Ndugumbi
      • Tandale
      • Wazo
    • Muundo wa utawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya utalii
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Matukio ya Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo cha mijini
  • Huduma zetu
    • Biashara
    • Huduma za Elimu
    • Maji na Usafishaji
    • Ujasiriamali na utoaji wa mikopo
    • Ushauri katika Kilimo
    • Elimu ya ufugaji, mifugo na uvuvi
    • Vituo vya Ukusanyaji Mapato
    • Vibali vya Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomiji na Mazingira
      • Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Baraza la Madiwani
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Makala
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Fomu za maombi
    • Vibali vya Ujenzi Vilivyotolewa
    • Nyaraka za Elimu
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Mifumo
    • NaPA
    • eMrejesho

KINONDONI YAAPISHA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA NA WAJUMBE WAKE

Tarehe iliyowekwa: December 2nd, 2019

Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mhe. Daniel Chongolo amewataka Wenyeviti wa Serikali za mitaa kuwa wadilifu katika kuwatumikia wananchi walio wachagua na kwamba waepuke kuwa miungu watu.

Mhe. Chongolo ametoa kauli hiyo leo wakati wa hafla ya kuapishwa kwa viongozi wa serikali za mitaa wa Halmashauri hiyo na kueleza kuwa kuapishwa kwao leo hakuwafanyi wakawe miungu watu kwa wananchi badala yake wakawatumikie kwa uadilifu.

Ameongeza kuwa suala la maslahi binafsi haliruhusiwi katika utendaji wao na kwamba hategemei kuona wenyeviti hao wanakwenda kinyume na maelekezo yanayotolewa.

“ Mmekula kiapo cha kwenda kutenda haki majukumu ya kuwatumikia wananchi, hamjala kiapo cha kwenda kuwa miungu watu, kuwa wabaguzi, hamjala kiapo ili mkawe watu wa kupendelea baadhi ya watu, na kuonea wengine"

Aidha Mhe. Chongolo amewaeleza kuwa kuna changamoto ya uonevu wa nyumba na mali za wanyonge hivyo kuwataka viongozi hao wa mitaa wakasimamie changamoto hizo.

 “ Kuna wananchi wanatapeliwa nyumba zao  na wajanja wajanja , ili wajimilikishe wao, kuanzia sasa nitasikitika sana hasa nikitambua nyinyi ambao leo hii ninawashuhudia mkila kiapo hapa mnakwenda kufanya mambo haya , nawaonya awamu hii sitawaacha, hatuwezi kukaa na watu wa hovyo, narudia hatuwezi kukaa na watu wa hovyo” amesisitiza Mhe. Chongolo.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Manispaa Ndugu. Aron Kagurumjuli amewataka wenyeviti wa serikali za mitaa kutumia vizuri madaraka waliyopewa na wananchi ili kuepusha mitafaruku ambayo ilikuwa ikijitokeza kwa baadhi ya wenyeweviti waliomaliza muda wao.

Amefafanua kuwa kazi ya wenyeviti wa serikali za mitaa hazina mishahara na kwamba inahitaji uzalendo mkubwa hivyo kuwataka watumie nafasi zao vizuri ili waweze kuendesha shuguli zao kwa ajili ya kuleta maendeleo kwa wananchi waliowachagua.

Aidha amewaonya wenyeviti hao kuacha mara moja tabia ya kuwatoza fedha wananchi pindi wanapotaka huduma  hivyo kuwaeleza kuwa huduma hizo zinapaswa kutolewa bure na kwamba atakayekwenda kinyume na maelekezo hayo hatamvumilia kwa namna yoyote ile.


Imetolewa na 

Kitengo Cha Habari na Uhusiano

 Manispaa ya Kinondoni.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI May 24, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MWENYEKITI WA BODI YA AJIRA April 13, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA DEREVA DARAJA II September 21, 2021
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI (TAREHE 20 SEPTEMBA, 2021) September 21, 2021
  • Tazama zote

Habari mpya

  • KINONDONI YAPONGEZWA KWA UJENZI WA KIWANJA CHA MICHEZO

    May 26, 2022
  • BARAZA LA MADIWANI ROBO YA TATU KINONDONI LAFANYIKA LEO

    May 18, 2022
  • KINONDONI KUFIKIA WATOTO TAKRIBANI 156871 KAMPENI YA SIKU NNE CHANJO YA POLIO KITAIFA

    May 18, 2022
  • MWENGE WA UHURU KINONDONI 2022, WAPITIA MIRADI YENYE THAMANI YA SHILINGI TAKRIBANI BILIONI 3.9 FEDHA ZA KITANZANIA

    May 10, 2022
  • Tazama zote

Picha Jongefu

POSHO MADIWANI
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • TARATIBU ZA KUPATA KIBALI CHA UJENZI
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • UJASIRIAMALI NA UTOAJI MIKOPO
  • VITUO VYA KUKUSANYIA MAPATO
  • ORODHA YA WAHESHIMIWA MADIWANI
  • RATIBA YA MSTAHIKI MEYA
  • TAARIFA KWA UMMA
  • MIRADI ILIYOKAMILIKA

Viunganishi Linganifu

  • TOVUTI KUU YA IKULU
  • TOVUTI YA UTUMISHI
  • TOVUTI YA OR-TAMISEMI
  • TOVUTI YA OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • TOVUTI YA IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

Idadi ya Wasomaji

world map hits counter

Waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Morogoro, 14883 Dar es Salaam

    Anuani ya Posta: S.L.P 31902

    Simu ya mezani: +255 22 2170173

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: md@kinondonimc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni. Haki Zote Zimehifadhiwa.