• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Kinondoni Municipal Council
Kinondoni Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Wasifu wa Halmashauri
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Afya na Usafishaji
      • Mipangomiji na Maendeleo ya Makazi
      • Kilimo na Mifugo
      • Elimu Sekondari
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA
    • Kata
      • Bunju
      • Hananasif
      • Kawe
      • Kigogo
      • Kijitonyama
      • Kinondoni
      • Kunduchi
      • Mabwepande
      • Magomeni
      • Makongo
      • Makumbusho
      • Mbezi Juu
      • Mbweni
      • Mikocheni
      • Msasani
      • Mwananyamala
      • Mzimuni
      • Ndugumbi
      • Tandale
      • Wazo
    • Muundo wa utawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya utalii
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Matukio ya Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo cha mijini
  • Huduma zetu
    • Biashara
    • Huduma za Elimu
    • Maji na Usafishaji
    • Ujasiriamali na utoaji wa mikopo
    • Ushauri katika Kilimo
    • Elimu ya ufugaji, mifugo na uvuvi
    • Vituo vya Ukusanyaji Mapato
    • Vibali vya Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomiji na Mazingira
      • Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Baraza la Madiwani
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Makala
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Fomu za maombi
    • Vibali vya Ujenzi Vilivyotolewa
    • Nyaraka za Elimu
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

KINONDONI! WEKENI MPANGO MKAKATI WA KUKUSANYA MADENI YATOKANAYO NA KODI YA ARDHI.

Tarehe iliyowekwa: October 19th, 2017

 NI AGIZO LA NAIBU WAZIRI WIZARA YA ARDHI ,NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI MH ANGELINA MABULA KATIKA KIKAO KAZI CHAKE NA WATENDAJI WA IDARA YA MIPANGOMIJI, ARDHI NA UTHAMINI MANISPAA YA KINONDONI.

 Manispaa ya Kinondoni imetakiwa kuweka mpango mkakati wa kuhakikisha inakusanya madeni yote yatokanayo na kodi ya Ardhi kwa wadaiwa sugu ili fedha hizo ziweze kutumika katika kuendeleza miradi ya Maendeleo. 

 Agizo hilo limetolewa leo na Naibu Waziri Wizara ya Ardhi Nyumba na maendeleo ya makazi Mh Angelina Mabula alipokuwa katika kikao kazi chake pamoja na watendaji kutoka Idara ya Mipangomiji, Ardhi na Uthamini kilichofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Manispaa. 

 Amesema ni vema ukawepo utaratibu mzuri wa kuhakikisha madeni na kodi hizi za Ardhi zinakusanywa ili fedha hizo ziweze kutumika katika kutekeleza miradi ya Maendeleo .

 "Wekeni Mapango mkakati wa kukusanya madeni, na madiwani hakikisheni mnapokaa kwenye vikao vyenu vya kila robo mmeletewa orodha ya wadaiwa waliopatiwa notisi kwa ajili ya malipo "Amesisitiza waziri .

Aidha amesema kikao kazi chake pamoja na mambo mengine ni kwa lengo la kukagua mfumo wa ukusanyaji mapato katika sekta ya Ardhi, kuangalia utendaji kazi wa mabaraza ya Ardhi pamoja na kuangalia namna ya kuendeleza maeneo yetu kupitia shirika la nyumba (NHC). 

 Naye katibu Tawala Wilaya Kinondoni Bi Gifti Msuya kwa Niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni katika taarifa yake kwa Naibu Waziri Wizara ya Ardhi amesema idara ya Mipangomiji inazo changamoto  ambazo zikifanyiwa kazi watakuwa katika hatua nzuri ya utekelezaji 

Amezitaja changamoto hizo kuwa ni ufinyu wa nafasi katika masijala ya ardhi, matumizi ya mfumo usiokuwa wa kielektroniki katika kutoa huduma, uwepo wa madalali na mwingiliano wa utekelezaji wa majukumu baina ya Wizara na Halmashauri. 

 Nyingine ni uvamizi wa maeneo, ujenzi holela, ufinyu wa bajeti katika kutoa fidia, wananchi kuwasilisha nyaraka za kughushi pamoja na ukusanyaji kodi maeneo yasiyopimwa. 

Katika hatua nyingine Mweyekiti wa baraza la Ardhi la Kinondoni Ndg Yose Mlyambina kwenye taarifa yake kwa Naibu waziri pia ameainisha changamoto za Baraza hilo la Ardhi kuwa ni kuchelewa kwa uteuzi wa wajumbe wa baraza, mfumo wa ulipaji wa ada za Halmashauri kutokuwa rafiki, ukosefu wa miongozo, uelewa mdogo wa sheria na taratibu za mahakama kwa wananchi pamoja na kuwa na mkanganyiko wa amri za utekelezaji kutoka kwa viongozi. 

 Hii ni mara ya kwanza kwa Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kutembelea Manispaa ya Kinondoni tangu kuteuliwa kwake kushika nyadhifa hiyo. 

 Imetolewa
 Kitengo cha Uhusiano
 Manispaa ya Kinondoni.

Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI KWA VITENDO (PRACTICAL) June 30, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA VITENDO KWA NAFASI YA DEREVA DARAJA II June 29, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO ULIOFANYIKA TAREHE 28 JUNI, 2022 June 28, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 20, 2022
  • Tazama zote

Habari mpya

  • UHUSIANO WA DSM NA HAMBURG WAFANIKISHA UZINDUZI KIWANDA CHA MBOJI

    June 30, 2022
  • VIKUNDI 286 VYA WANUFAIKA WA MIKOPO YA ASILIMIA 10 VYAPATIWA MAFUNZO

    June 20, 2022
  • MAFUNZO KAZI YA MFUMO WA UTOAJI, USIMAMIZI WA MIKOPO YA ASILIMIA 10

    June 18, 2022
  • KINONDONI YAPONGEZWA KWA UJENZI WA KIWANJA CHA MICHEZO

    May 26, 2022
  • Tazama zote

Picha Jongefu

UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • TARATIBU ZA KUPATA KIBALI CHA UJENZI
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • UJASIRIAMALI NA UTOAJI MIKOPO
  • VITUO VYA KUKUSANYIA MAPATO
  • ORODHA YA WAHESHIMIWA MADIWANI
  • RATIBA YA MSTAHIKI MEYA
  • TAARIFA KWA UMMA
  • MIRADI ILIYOKAMILIKA

Viunganishi Linganifu

  • TOVUTI KUU YA IKULU
  • TOVUTI YA UTUMISHI
  • TOVUTI YA OR-TAMISEMI
  • TOVUTI YA OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • TOVUTI YA IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

Idadi ya Wasomaji

world map hits counter

Waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Morogoro, 14883 Dar es Salaam

    Anuani ya Posta: S.L.P 31902

    Simu ya mezani: +255 22 2170173

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: md@kinondonimc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni. Haki Zote Zimehifadhiwa.