• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Kinondoni Municipal Council
Kinondoni Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Wasifu wa Halmashauri
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Afya na Usafishaji
      • Mipangomiji na Maendeleo ya Makazi
      • Kilimo na Mifugo
      • Elimu Sekondari
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA
    • Kata
      • Bunju
      • Hananasif
      • Kawe
      • Kigogo
      • Kijitonyama
      • Kinondoni
      • Kunduchi
      • Mabwepande
      • Magomeni
      • Makongo
      • Makumbusho
      • Mbezi Juu
      • Mbweni
      • Mikocheni
      • Msasani
      • Mwananyamala
      • Mzimuni
      • Ndugumbi
      • Tandale
      • Wazo
    • Muundo wa utawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya utalii
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Matukio ya Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo cha mijini
  • Huduma zetu
    • Biashara
    • Huduma za Elimu
    • Maji na Usafishaji
    • Ujasiriamali na utoaji wa mikopo
    • Ushauri katika Kilimo
    • Elimu ya ufugaji, mifugo na uvuvi
    • Vituo vya Ukusanyaji Mapato
    • Vibali vya Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomiji na Mazingira
      • Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Baraza la Madiwani
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Makala
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Fomu za maombi
    • Vibali vya Ujenzi Vilivyotolewa
    • Nyaraka za Elimu
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI KINONDONI YATEMBELEA WADAU KUTOKA ASASI ZA KIRAIA

Tarehe iliyowekwa: October 27th, 2021

Kamati hiyo chini ya Mwenyekiti wake ambaye pia ni Naibu Meya wa Manispaa hiyo na diwani wa Kata ya Bunju Mhe. Kheri Misinga imetembelea Asasi ya "YCR" pamoja na "LHRO" kwa lengo la kujiridhisha na utekelezaji wa  shughuli zihusuzo mapambano dhidi ya dawa za kulevya kwa vijana pamoja na VVU na UKIMWI, lakini pia kujiridhisha na njia zitumiwazo katika kufikisha elimu na ujumbe sahihi kwa walengwa.

Mhe. Misinga amesema dhana nzima ya ziara hiyo pia ni kuweka msingi imara na mpango mkakati wa jinsi ya kushirikiana kwa pamoja na Asasi za kiraia katika kuhakikisha Afua za VVU na UKIMWI pamoja na mapambano dhidi ya dawa za kulevya zinatekelezwa kwa kiwango kilichokusudiwa hali itakayoleta tija kwa Taifa letu.

"Asasi za kiraia ni wadau muhimu sana katika Halmashauri yetu, kwani tunashirikiana nao kwa karibu sana katika kuhakikisha mapambano dhidi ya VVU na UKIMWI, pamoja na dawa za kulevya yanafanyika kwa kiasi kikubwa. Wenzetu hawa wanazo njia tofauti za kuwafikia walengwa kwa ukaribu, hivyo tuendelee kushirikiana nao, nisisitize pia tunapotoa elimu juu ya VVU na UKIMWI pamoja na madawa ya kulevya tukumbuke na hili janga la UVIKO-19," Amesema Misinga.

Alipokuwa akijibu suala la UVIKO-19, Mganga Mkuu wa Manispaa ya Kinondoni Ndg. Samweli Laizer amesema kupitia Mpango wa Maendeleo kwa Ustawi wa Taifa na mapambano dhidi ya UVIKO-19 unaoratibiwa na Serikali kupitia Wizara ya Fedha, Kinondoni imejipanga kutekeleza shughuli hiyo kwa kushirikiana na wadau mbalimbali lengo likiwa ni kufikia wananchi wengi kwa wakati sahihi.

Aidha Dkt. Laizer amesema kuwa ni vema kupata chanjo ya UVIKO-19, kwa hiari kwani ni bora kuliko tiba na kuwataka wananchi kuondokana na dhana potofu zihusianazo na ugumba kwa wanawake na nguvu za kiume.

Naye Mratibu wa kudhibiti UKIMWI Manispaa ya Kinondoni Bi. Rhobi Gweso alipokuwa akizungumza amesema, Kinondoni imekuwa ikishirikiana na Asasi hizi kwa ukaribu sana lengo likiwa ni kusaidiana kwa pamoja kufikia lengo tarajiwa la kupunguza maambukizi katika jamii.

Ziara hiyo imehudhuriwa pia na Wakuu wa Idara na Vitengo, wawakilishi wa makundi ya dini, vijana, wazee na watu wenye ulemavu.

Imeandaliwa na

Kitengo Cha Habari na Uhusiano

Manispaa ya Kinondoni.

Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA VITENDO KWA NAFASI YA DEREVA DARAJA II June 29, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO ULIOFANYIKA TAREHE 28 JUNI, 2022 June 28, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MWENYEKITI WA BODI YA AJIRA April 13, 2022
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIKUNDI 286 VYA WANUFAIKA WA MIKOPO YA ASILIMIA 10 VYAPATIWA MAFUNZO

    June 20, 2022
  • MAFUNZO KAZI YA MFUMO WA UTOAJI, USIMAMIZI WA MIKOPO YA ASILIMIA 10

    June 18, 2022
  • KINONDONI YAPONGEZWA KWA UJENZI WA KIWANJA CHA MICHEZO

    May 26, 2022
  • BARAZA LA MADIWANI ROBO YA TATU KINONDONI LAFANYIKA LEO

    May 18, 2022
  • Tazama zote

Picha Jongefu

POSHO MADIWANI
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • TARATIBU ZA KUPATA KIBALI CHA UJENZI
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • UJASIRIAMALI NA UTOAJI MIKOPO
  • VITUO VYA KUKUSANYIA MAPATO
  • ORODHA YA WAHESHIMIWA MADIWANI
  • RATIBA YA MSTAHIKI MEYA
  • TAARIFA KWA UMMA
  • MIRADI ILIYOKAMILIKA

Viunganishi Linganifu

  • TOVUTI KUU YA IKULU
  • TOVUTI YA UTUMISHI
  • TOVUTI YA OR-TAMISEMI
  • TOVUTI YA OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • TOVUTI YA IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

Idadi ya Wasomaji

world map hits counter

Waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Morogoro, 14883 Dar es Salaam

    Anuani ya Posta: S.L.P 31902

    Simu ya mezani: +255 22 2170173

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: md@kinondonimc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni. Haki Zote Zimehifadhiwa.