• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Kinondoni Municipal Council
Kinondoni Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Wasifu wa Halmashauri
  • Utawala
    • Divisheni
      • Miundombinu, Vijijini na Mijini
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Fedha na Mahesabu
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Manunuzi
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
    • Kata
      • Bunju
      • Hananasif
      • Kawe
      • Kigogo
      • Kijitonyama
      • Kinondoni
      • Kunduchi
      • Mabwepande
      • Magomeni
      • Makongo
      • Makumbusho
      • Mbezi Juu
      • Mbweni
      • Mikocheni
      • Msasani
      • Mwananyamala
      • Mzimuni
      • Ndugumbi
      • Tandale
      • Wazo
    • Muundo wa Taasisi
    • Ofisi ya Mtendaji wa Kata
    • Ofisi ya Mtendaji wa Mtaa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya utalii
      • Fukwe na Visiwa
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
    • Utalii
      • Matukio ya Utalii
      • Royal Tour Bus
  • Huduma zetu
    • Biashara
    • Huduma za Elimu
    • Ujasiriamali
    • Ushauri katika Kilimo
    • Vituo vya Ukusanyaji Mapato
    • Vibali vya Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomiji na Mazingira
      • Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Fomu za maombi
    • Vibali vya Ujenzi Vilivyotolewa
    • Nyaraka za Elimu

DC CHONGOLO ATAKA USAWA KWA WATU WENYE ULEMAVU, ASEMA WASINYANYAPALIWE

Tarehe iliyowekwa: November 15th, 2019

Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Mhe. Daniel Chongolo ameiasa jamii kutojihusisha na tabia ya kuwanyanyapaa watu wenye ulemavu kwakuwa na wao wana haki ya kupata haki zote kama ilivyo kwa watu wengine.

Mhe. Chongolo ametoa kauli hiyo leo wakati wa uzinduzi wa kamati ya watu wenye ulemavu uliofanyika Manispaa ya Kinondoni ambapo pamoja na mambo mengine amesema ipo dhana iliyojengeka ya kuwanyanyapaa watu hao na hivyo kueleza kuwa kufanya hivyo ni makosa na kusisitiza kuwa nilazima itendeke haki na usawa.

Amesisitiza kuwa watu wenye ulemavu wanahaki ya kupewa nafasi mbalimbali na kusema kuwa wote wenye dhamana ya uongozi katika Halmashauri hiyo ni lazima kuangalia makundi hayo kwa upekee zaidi kwa kutenda haki na usawa.

Mhe. Chongolo amefafanua kuwa ili kufikia malengo hayo kila mmoja hakuna budi kushirikiana na kamati hiyo iliyoundwa kuweka miundombinu sawia itakayowezesha walemavu kuishi kwa kupata haki zao na usawa pamoja na kuepusha kunyanyapaliwa kama ilivyo kwa sasa.

“ Nawashukuru sana kwakunipa heshima hii ya kuzindua kamati hii ambayo inalenga kusimamia, kushughulikia ipasavyo kutetea haki na usawa wawatu wenye ulemavu” amesema Mhe. Chongolo.

Mhe. Chongolo hakusita kueleza changamoto mbalimbali zilizopo katika  Halmashauri ya Kinondoni na kusema kuwa sio vijijini tu hata mijini wapo baadhi ya watu wanao wanyanyapaa walemavu kwakuwatenga, kuwaficha pamoja na kuwanyima fursa yakupatiwa huduma kama watu wengine.

“ Jamii imekuwa na taswira mbaya yakuona kwamba ulemavu ni changamoto iliyokuwa na madhara , na hivyo kujikita kunyanyapaa, kamati hii imepewa mamlaka, sasa nendeni mkajenge timu nzuri itakayoleta sura ya kubadilisha mtazamo uliopo hivi sasa na kuleta matunda na faida kwao.

Awali taarifa ya watu wenye ulemavu, ilieleza kuwa halmashauri inajumla ya kata 20 ambazo zinahudumia watu hao wapatao 1239 ambapo kati yao wanaume ni 724 na wanawake 515.

Aidha taarifa hiyo ilieleza kuwa kati ya watu hao wakubwa ni 973 huku watoto wakiwa 266 na kwamba huduma hizo zinatolewa kwakuzingatia sera ya watu wenye ulemavu ya mwaka 2004, sheria namba 9 ya mwaka 2010 pamoja na mikataba mbalimbali inayohusu watu wenye ulemavu.

Ameeleza kuwa , Halmashauri imekuwa ikiviwezesha vyama vya watu wenye ulemavu kwa kuvipatia vifaa saidizi kulingana na aina ya ulemavu sambamba na kuwapatia misaada au kujikimu kwa walio na mazingira hatarishi.

Aidha ameeleza kuwa , Kinondoni imekuwa ikiwaunganisha na asasi za kiraia ili waweze kujipatia ujuzi , ajira na misaada ya kujikumu palipo na uhitaji pamoja na kuwawezesha maadhimisho ya watu wenye ulemavu yanayofanyika kila mwaka.


Imeandaliwa na

Kitengo cha Habari na Uhusiano

Manispaa ya Kinondoni.

Matangazo

  • UTOAJI WA MIKOPO KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU April 01, 2025
  • TANGAZO March 22, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 05, 2024
  • MATOKEO YA USAILI WA VITENDO KADA YA AFISA TEHAMA MSAIDIZI ULIOFANYIKA TAREHE 25/03/2024 March 25, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • ZAIDI YA MITI 1200 YAPANDWA KUADHIMISHA MIAKA 63 YA UHURU

    December 09, 2024
  • MAAMBUKIZI UKIMWI YAPUNGUA

    December 01, 2024
  • MAAMBUKIZI YA VIRUSI VYA UKIMWI YASHUKA KINONDONI

    November 29, 2024
  • WENYEVITI NA WAJUMBE WAPYA WAPEWA MAELEKEZO YA MAJUKUMU YAO

    November 28, 2024
  • Tazama zote

Picha Jongefu

IFAHAMU KATA YA MZIMUNI, MANISPAA YA KINONDONI
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MWONGOZO WA NAMNA YA KUTUMIA MFUMO WA TAUSI
  • UJASIRIAMALI NA UTOAJI MIKOPO
  • MAKTABA YA PICHA
  • TAARIFA KWA UMMA
  • HOTUBA
  • ORODHA YA WAHESHIMIWA MADIWANI
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MIRADI ILIYOKAMILIKA

Viunganishi Linganifu

  • TOVUTI KUU YA IKULU
  • TOVUTI YA UTUMISHI
  • TOVUTI YA OR-TAMISEMI
  • TOVUTI YA OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • TOVUTI YA IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

Idadi ya Wasomaji

world map hits counter

Waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Morogoro, 14883 Dar es Salaam

    Anuani ya Posta: S.L.P 31902

    Simu ya mezani: +255222170173

    Simu ya mkononi: +255733241052

    Barua pepe: md@kinondonimc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni. Haki Zote Zimehifadhiwa.