• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Kinondoni Municipal Council
Kinondoni Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Wasifu wa Halmashauri
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Afya na Usafishaji
      • Mipangomiji na Maendeleo ya Makazi
      • Kilimo na Mifugo
      • Elimu Sekondari
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA
    • Kata
      • Bunju
      • Hananasif
      • Kawe
      • Kigogo
      • Kijitonyama
      • Kinondoni
      • Kunduchi
      • Mabwepande
      • Magomeni
      • Makongo
      • Makumbusho
      • Mbezi Juu
      • Mbweni
      • Mikocheni
      • Msasani
      • Mwananyamala
      • Mzimuni
      • Ndugumbi
      • Tandale
      • Wazo
    • Muundo wa utawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya utalii
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Matukio ya Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo cha mijini
  • Huduma zetu
    • Biashara
    • Huduma za Elimu
    • Maji na Usafishaji
    • Ujasiriamali na utoaji wa mikopo
    • Ushauri katika Kilimo
    • Elimu ya ufugaji, mifugo na uvuvi
    • Vituo vya Ukusanyaji Mapato
    • Vibali vya Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomiji na Mazingira
      • Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Baraza la Madiwani
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Makala
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Fomu za maombi
    • Vibali vya Ujenzi Vilivyotolewa
    • Nyaraka za Elimu
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono

Kijiji cha Makumbusho

Kijiji cha Makumbusho kilichopo pembezoni ya barabara ya Ally Hassan Mwinyi nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam katika Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni kilianzishwa mwaka 1996 kwa lengo la kuhifadhi na kuonyesha tamaduni mbalimbali za makabila ya Kitanzania.

Kijiji cha Makumbusho ni kivutio kizuri cha utalii kinachoonesha tamaduni za makabila yasipungua 100 ya Tanzania. Kinazo nyumba za asili zilizojengwa kwa tope na kuezekwa kwa nyasi na tope. Vivevile kina michoro ya asili, mikeka iliyosukwa kwa mikono na ngoma za asili zinazovutia kucheza.

Makumbusho haya yamehifadhi na kuonyesha namna yalivyo makazi mbalimbali ya Watanzania kote nchini na pia hutoa fursa kwa wageni kusikiliza ngoma za asili kutoka makabila tofauti tofauti.

Kutembelea Kijiji cha Makumbusho ni sawa na kuitembelea Tanzania nzima ndani ya muda mfupi, kwa kuweza kuona na kujifunza juu ya tamaduni za makabila mbalimbali yaliyopo Tanzania.

Wageni na wenyeji pia wanapata fursa ya kula vyakula mbalimbali vya asili na kuburudika na ladha yake murua, pamoja na wasaa wa kufanya manunuzi ya bidhaa tofauti tofauti za kiutamaduni.

Nyumba za asili katika Kijiji cha Makumbusho


Nyumba ya Sanaa

Mahali pekee pa kuona kazi za wasanii na kugundua vipaji vyao vya kipekee katika sanaa za kitamaduni ni katika Nyumba ya Sanaa inayopatikana katika mtaa wa Ohio karibu na Hoteli ya Movenpick.

Maonyesho ya nyimbo za kitamaduni huchezwa kila Ijumaa. Ngoma na nyimbo za asili huchezwa kwa ala za muziki kutoka kwa vikundi vya Simba Theatre International, Super Kamambe na Sisi Tambala.

Kituo hiki kinakaribisha wenyeji na wageni mbalimbali kujionea na kuburudika kwa kazi za wasanii na urithi wa kitamaduni wa Jiji la Dar es Salaam na Tanzania kwa ujumla.

Nyumba ya Sanaa


Mwenge Vinyago

Pembezoni tu mwa Jiji, katika barabara ya kuelekea Bagamoyo, mwendo wa takribani dakika 45 kutoka katikati ya Jiji, kuna Soko la Wachongaji vinyago cha Mwenge maarufu kama Mwenge vinyago ambalo lilianzishwa mnamo mwaka 1984. Vinyago hivi vinavyochongwa vizuri kabisa vinakuwa katika muonekano na ukubwa tofauti tofauti.

Kituo cha Wachongaji vinyago Mwenge kimekua na wanachama wa chama cha wachongaji vinyago wa Tanzania. Mwenge vinyago ina soko linalojumuisha maduka madogo na fremu zinazoonyesha na kuuza sio tu vinyago lakini pia nguo za kitamaduni, kanga, vikoni na picha za tinga tinga. Vinyago vinachongwa kwa kutumia mti wa Mpingo, Mkangazi na Mwarobaini.

Katika Mwenge Vinyago kuna jamii kubwa ya wachongaji vinyago na wachoraji wakiwa sura za bashasha wakitekeleza majukumu yao kwa bidii na ufanisi mkubwa.

Wageni mbalimbali wanapata fursa ya kujionea namna vinyago vinavyotengenezwa ikiwa ni pamoja na kuzungumza na wasani hao kuhusu maisha yao na mazingira kwa ujumla.

Kwa manunuzi yote ya vinyago na picha za rangi za kuvutia. Mwenge vinyago ndiyo suluhisho.


Michoro ya Tingatinga

Hivi pia ni maarufu sana Tanzania, ni mtindo wa kupaka rangi wa Tingatinga. Mtindo huu ambao hutokana na kutumia rangi za mafuta na kutengeneza michoro ya katuni, huvutia sana. Usiondoke Dar es Salaam kabla haujanunua Tingatinga na uweke kwenye fremu ufikapo nyumbani. Utapata aina nyingi katika Kituo cha sanaa Tingatinga.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI May 24, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA DEREVA DARAJA II September 21, 2021
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI (TAREHE 20 SEPTEMBA, 2021) September 21, 2021
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIKUNDI 286 VYA WANUFAIKA WA MIKOPO YA ASILIMIA 10 VYAPATIWA MAFUNZO

    June 20, 2022
  • MAFUNZO KAZI YA MFUMO WA UTOAJI, USIMAMIZI WA MIKOPO YA ASILIMIA 10

    June 18, 2022
  • KINONDONI YAPONGEZWA KWA UJENZI WA KIWANJA CHA MICHEZO

    May 26, 2022
  • BARAZA LA MADIWANI ROBO YA TATU KINONDONI LAFANYIKA LEO

    May 18, 2022
  • Tazama zote

Picha Jongefu

POSHO MADIWANI
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • TARATIBU ZA KUPATA KIBALI CHA UJENZI
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • UJASIRIAMALI NA UTOAJI MIKOPO
  • VITUO VYA KUKUSANYIA MAPATO
  • ORODHA YA WAHESHIMIWA MADIWANI
  • RATIBA YA MSTAHIKI MEYA
  • TAARIFA KWA UMMA
  • MIRADI ILIYOKAMILIKA

Viunganishi Linganifu

  • TOVUTI KUU YA IKULU
  • TOVUTI YA UTUMISHI
  • TOVUTI YA OR-TAMISEMI
  • TOVUTI YA OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • TOVUTI YA IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

Idadi ya Wasomaji

world map hits counter

Waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Morogoro, 14883 Dar es Salaam

    Anuani ya Posta: S.L.P 31902

    Simu ya mezani: +255 22 2170173

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: md@kinondonimc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni. Haki Zote Zimehifadhiwa.